Meli iliyo zama - Picha na Nathan Chiume
Kwa niaba
ya Jumuiya ya Watanzania, na Watanzania wote tunaoishi nchini Japan naomba
niwajulishe kwamba tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya
ajali ya meli ya MV SKAGIT,
iliyokuwa
ikisafiri kutoka Dar kuelekea Zanzibar, ambayo imesababisha wenzetu wengi
kupoteza
maisha na
wengine kujeruhiwa.
Tunawapongeza na kuwashukuru taasisi mbali-mbali na watu binafsi
wanaofanya kazi kubwa kukabili
zoezi la
uokoaji, na wale waliotufikishia habari hizi. Tunawashukuru wale wote waliopata
taarifa na
kuelekea
kwenye eneo la tukio na kuanza uokoaji mara moja.
Uongozi
wa Jumuiya ya Watanzania, na Watanzania wote tunaoishi nchini Japan, tuko pamoja
nanyi,
na pia
tunaungana na Watanzania wenzetu wote kutoa pole kwa wafiwa, na kuwaombea
majeruhi waweze
kupona
kwa haraka. Tunamuomba Mwenyezi Mungu aziweke pema peponi roho za marehemu wote
na
kuwapa
nguvu na uvumulivu ndugu na jamaa, katika kipindi hiki
kigumu.
NJENGA,
Rashid
Mwenyekiti,
Jumuiya ya
Watanzania Waishio nchini Japan.
No comments:
Post a Comment