KAMA OPTION

KAMA OPTION

KI

KI

eid

eid

Monday, August 17, 2009

Mashindano ya Karate









Mtanzania, Karateka Yassir Kiluke mwenye shati jeupe atashiriki kwenye mashindano ya Karate yatakayofanyika kwenye ukumbi wa Keio Plaza Hotel huko Hachioji kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 11 jioni siku ya tarehe 23 Agosti 2009.
Watanzania wote pamoja na marafiki wengine mnakaribishwa kuhudhuria mashindano hayo kujua kinachojiri na pia kumuunga mkono mwenzetu ambaye amejitosa katika mchezo huu maarufu wa self-defence nchini Japani.
Keio Plaza Hotel iko kiasi cha dakika mbili kutoka kituo cha treni cha Hachioji.



2 comments:

Mbele said...

Nikiwa ni mdau sugu wa blogu yako, nakushukuru kwa taarifa unazoleta kuhusu shughuli za Watanzania huko Japani. Kila la heri.

Mzee wa Changamoto said...

Hapa ni mahala tunapojumuika kujua yanayojiri upande wa Japan na hasa kwa waTanzania waishio na wajishughulishao na mambo mbalimbali huko.
Na sasa waendeleza kwa kutuunganisha na Kaka Yassir Kiluke. Twamtakia mpambano mwema hiyo kesho na twaamini atafanikisha ndoto zake
Nawe twakushukuru na twakutakia kila lililo jema