TAARIFA YA MSIBA
Ndugu watanzania wenzangu,Mtanzania mwenzetu Bw. Rajabu Urembo wa Sagamihara amepatwa na msiba wakuondokewa na mama yake Zainabu binti Pazi uliotokea siku ya Jumatano tarehe 19/5/2010huko Vingunguti, Dar es salaam.Kama ilivyo kawaida yetu naomba tuchukue fursa hii kumpa pole na kumfariji mwenzetuwakati wa kipindi hiki kigumu.Unaweza kuwasiliana na Bw. Urembo kwa simu namba: 080-3936-4813.Taarifa zaidi kuhusu kisomo cha kumuombea marehemu na taarifa zingine zitafuata baadaye.Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi, Amen.
Ahsanteni
Simba
Mwenyekiti,
Jumuiya ya Watanzania Wanaoishi Nchini Japani.
No comments:
Post a Comment