KAMA OPTION

KAMA OPTION

KI

KI

eid

eid

Monday, August 11, 2008

JUMUIYA YAPATA VIONGOZI





Viongozi wapya wa Jumuiya ya Watanzania wanaoishi nchini Japan jana Jumapili wameitisha mkutano wao kwanza wa Watanzania wote kujadili mambo mbali mbali yanayohusiana na Jumuiya ya Watanzania hapa Japan pamoja na kujaza nafasi za mweka hazina wa Jumuiya na makamu wake na wajumbe wa kamati mbali mbali.



Viongozi hao wapya wa Jumuiya Dr.Ally Yahaya Simba(mwenyekiti),Bw. Andrew Kapinga (makamu mwenyekiti),Bw.Julius Mwombeki(katibu mkuu),Bw.Abby Senkoro(naibu katibu mkuu)walichaguliwa katika mkutano mkuu wa Watanzania wote uliofanyika tarehe 27 Julai 2008.Katika mkutano wa jana wajumbe waliwachagua Bw.Juma Kipaya(mweka hazina)na Bi. Fatma Mbilili(naibu mweka hazina).

No comments: