Taatifa ya Kisomo
Ndugu viongozi na wajumbe,Naomba niwape taarifa za kisomo za Msiba wa Mama wa Ndugu yetu Eddie Samata (Eddie Mpemba) wa Fujisawa, Kanagawa-ken.Bw. Eddie alifiwa na Mama yake mzazi huko Tanzania na mazishi yalifanyika Tarehe 2 Julai.Bw. Eddie amesharudi Japan na tutakuwa na Kisomo cha kumkumbuka Mama yetu hapo Tarehe 11 Agosti 2013 kuanzia saa kumi jioni (4:00pm) katika ukumbi wa mikutano Tsuruma mkabala na ItoYokado shopping Mall.Ninaomba wajumbe wa kamati ya Raha na shida tushirikiane katika shughuli hii.Pia naomba wajumbe wa kamati ya habari tutoe tangazo hili kwenye vyombo vyetu, ili watanzania wote waweze kupata habari hii.Roho ya Marehemu ipate rehema kwa Mungu ipumzike kwa amani, Amina.
David P. Semiono
MwenyekitiTanzanite Society
No comments:
Post a Comment