MATEMBEZI YA HISANI (60TH YOKOHAMA INTERNATIONAL
COSTUME PARADE, ALHAMISI TAREHE 3 MAY 2012
Ubalozi wa Tanzania nchini Japani unapenda kuwajulisha
Watanzania wote waishio Tokyo, maeneo ya karibu na Tokyo na Japan kwa ujumla
kuwa Mji wa Yokohama unaandaa matembezi ya Hisani (60th Yokohama International
Costume Parade) tarehe 03/05/2012 au tarehe 04/05/2012 endapo kutakuwa na mvua
tarehe 3.
Kwa mara ya kwanza maonyesho hayo
yaliandaliwa na mji wa Yokohama mwaka 1953 kwa lengo la kuhamasisha jitihada za
kufufua uchumi na utalii wa mji wa Yokohama kufuatia uharibifu ulitokana na Vita
Kuu vya Pili vya Dunia (WWII). Kutoka kuasisiwa kwake maonyesho haya yamekuwa
yakipata umaarufu mwaka hadi mwaka.
Katika
matembezi ya mwaka 2012, Ubalozi umejulishwa na Kamati ya maandalizi kuwa
Tanzania imechaguliwa na kuombwa kushiriki katika matembezi hayo. Maombi hayo
yalifafanua zaidi kuwa Tanzania imechaguliwa na kuombwa kushiriki katika
matembezi hayo kutokana na historia yake ya kupenda,kusimamia na kutetea amani,
umoja na mshikamano duniani.
Sababu nyingine
ni kuwa Mji wa Yokahama una nia ya kuanzisha uhusiano (Sistercity Friendship) na
mojawapo ya miji ya Tanzania katika siku za karibuni. Uhusiano ambao utajumuisha
kupanda miti aina ya cherry blossom katika mji utakaochaguliwa
Tanzania.
Hivyo matembezi hayo yanalenga
pamoja na kuendeleza mshikamano wa watu wa Yokohama, yatatumika kuitangaza
Tanzania, hususan mila na desturi za Mtanzania (amani, umoja na
mshikamano).
Ili kuonyesha umoja na
mshikamano wetu wa Tanzania, Ubalozi unapenda kuwaalika Watanzania wote waliopo
Japan kujitokeza kwa wingi kushiriki matembezo hayo ya hisani. Aidha, katika
kuainisha utamaduni wetu ni muhimu kuvaa mavazi ambayo yataelezea utanzania,
mfano khanga kwa kina mama/dada na rubega kwa kina baba/kaka
n.k.
Muda, Mahali na
UmbaliMatembezi yatafunguliwa rasmi saa 4.45 (nne na dakika
arobaini na tano) asubuhi mbele ya Hotel New
Grand.
Matembezi hayo yatatanguliwa na
matembezi ya watoto (Kid’s Parade) saa 4:45 (nne na dakika arobaini na tano)
asubuhi, Yamashita Park-Red Brick Warehouse-Makutano ya Bankokubashi, ubali ni
Km 1.4
Saa 5:15 (tano na robo) asubuhi,
matembezi ya watu wazima (Super Parade) yataaza (Yamashita Park-Red Brick
Warehouse- Bashamichi shopping avenue-Isesaki-cho 6 chome- umbali ni Km
3.4
Kwa wote watakaopenda kushiriki, tunaomba
watume majina yao na mawasiliano yako kwenye barua pepe
zifuatazo:tzrepjp@gol.com, fmossongo@tanzaniaembassy.or.jp
jmaleko@tanzaniaembassy.or.jp
Ushiriki wa
Tanzania katika matembezi hayo utaongozwa na Mhe. Salome T.
Sijaona, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Japan.Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania Tokyo, Japan
No comments:
Post a Comment